Tuesday 30 April 2013

KESI YA MAUAJI PADRE MUSHI ZANZIBAR YAENDELEYA !!!


Jaji wa Mahakama Kuu, Mkusa Isaack Sepetu.
Mahakama Kuu ya Zanzibar imetupilia mbali ombi la mtuhumiwa wa mauaji ya Padre Evarist Mushi, la kupinga kukamatwa na kushikiliwa kwa zaidi ya saa 24 bila ya kupelekwa mahakamani, kutokana na ombi hilo kufunguliwa kinyume na sheria za Zanzibar.

Mtuhumiwa Omar Mussa Makame (35), alifungua ombi hilo mahakamani kupitia jopo la mawakili wanaomtetea Abdallah Rajab Abdallah na Abdallah Juma Mohamed.

Mawakili hao walikuwa wakipinga kitendo cha Jeshi la Polisi Zanzibar kumkamata mtuhumiwa huyo Machi 17, mwaka huu na kufikishwa mahakamani Aprili 5, mwaka huu.

Akisoma hukumu baada ya kusikiliza ombi hilo, Jaji wa Mahakama Kuu, Mkusa Isaack Sepetu, alisema ombi hilo lilifunguliwa kinyume na kifungu cha nne Sura ya 28 cha Sheria ya Zanzibar.

Aidha, Jaji Mkusa alisema maombi hayo yameonekana kuwa na tarehe mbili tofauti, ikiwamo mwezi Machi na Aprili na hivyo kuipa wakati mgumu mahakama kufahamu ni tarehe ipi ambayo hati ya kiapo ilifunguliwa kabla ya kusikilizwa na kutolewa uamuzi wake.

“Kutokana na kasoro hizo za kisheria, maombi hayo hayakuwa na nguvu za kisheria, kujadiliwa na kutolewa maamuzi na kwa msingi huo,  Mahakama imeyatupa,” alisema Jaji Mkusa.

Hata hivyo, wakati hukumu hiyo inasomwa, mawakili wote wanaomtetea mshtakiwa huyo hawakuwapo na wakati Jaji Mkusa, akijitayarisha kupanga tarehe ya kutajwa kesi ya msingi, wakili kutoka kampuni ya A.J.M Shaban Juma Shaban, alifika ghafla katika ukumbi wa mahakama na kuitaka mahakama kurejea hatua ya mwenendo wa kesi ilipofikia.

Jaji Mkusa aliwataka mawakili hao kuwa makini wanapotekeleza majukumu yao, kwa vile kampuni hiyo ina mawakili wengi na hakukuwa na sababu za msingi za kutofika wakili hata mmoja wakati wakifahamu kesi ya msingi itatajwa pamoja na kutolewa hukumu ya ombi la mteja wao.

“Natoa nafasi kwa upande wa Mwendesha Mashitaka, kurudia maelezo aliyoyatoa mahakamani kuhusu kesi ya msingi, lakini tabia hiyo iwe mwanzo na mwisho,” alisema Jaji Mkusa.

Aidha, Jaji Mkusa aliwataka mawakili hao kutorudia hoja wanazoziwasilisha mahakamani na kutolewa uamuzi ili kuepusha mahakama hiyo kuwa kama gurudumu la kujadili mambo ambayo yameshajadiliwa na kutolewa uamuzi wake.

Hatua hiyo imekuja baada ya Wakili Shabani kutaka mahakama hiyo imwachie huru mtuhumiwa huyo kama upelelezi bado haujakamilika pamoja na kutaka Mmhakama iwape muda maalum wa kuhakikisha upelelezi unakamilika, hoja ambazo zimewahi kuwasilishwa na Wakili Abdallah Juma Mohamed Aprili 19, mwaka huu.

Awali, Mwendesha Mashitaka kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka, Abdallah Issa Mgongo, aliieleza mahakama hiyo kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Mgongo alisema uchunguzi wa kesi hiyo bado haujakamilika na hivyo kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kusikilizwa kwa shauri hilo, lakini wakati akitoa maelezo hayo mawakili wa mtuhumiwa hawakupo katika ukumbi wa mahakama hiyo.

Jaji Mkusa aliiahirisha kesi hiyo hadi Mei 9 mwaka huu na kuwataka wahusika wote kuhakikisha wanafika kwa wakati ili kuepusha usumbufu wowote kama ulivyojitokeza jana.

BEATRIX TEKENT ABDICATIE,WILLEM-ALEXANDER NIEUWE KONING!!!


Prinses Beatrix heeft dinsdagochtend met het tekenen van de Akte van Abdicatie afstand gedaan van de troon. Willem-Alexander is de nieuwe koning van Nederland.

ANP
In de Vroedschapskamer van het Koninklijk Paleis, ook wel de Mozeszaal genoemd, tekende Beatrix na een korte toespraak de Akte van Abdicatie waarmee zij na 33 jaar koningsschap weer prinses is geworden en haar oudste zoon koning. Ook Willem-Alexander en koningin Maxima tekenden het document.
Prinses Amalia is vanaf nu troonopvolgster. Zij heeft de titel 'Prinses van Oranje' gekregen.
Op het moment dat de handtekeningen werden gezet ging er luid gejuich op op de Dam. Het plein voor het paleis, waar de ceremonie op groot scherm is te volgen, staat helemaal vol. Volgens de politie zijn er 25.000 mensen aanwezig. 
Bij de plechtigheid in het paleis op de Dam in Amsterdam zijn naast leden van de koninklijke familie 31 getuigen aanwezig. Die ondertekenen ook de Akte van Abdicatie. Het perkamenten document wordt voorzien van het grootzegel en later in de Nieuwe Kerk tentoongesteld.
Kwa ufupi kwa wale wasio fahamu hii lugha,kuwa mama mwenye nchi leo hii amestaafu kuingoza Holland na amemkabizi mwanawe Willem -Alexander kuwa kiongozi mpya Koning van Nederland   

KISHINDO KATIBA MPYA ,LENGO NI ZANZIBARI KOTOKUWA NA MAMLAKA KAMILI !!!

*Jaji Warioba atangaza msimamo mzito
*Asema tume itaingilia mawazo ya wananchi 


Jaji Joseph Warioba
TUME ya Mabadiliko ya Katiba, imesema italazimika kuingilia mawazo ya wananchi, kwa kuyaacha baadhi ya mapendekezo yaliyotolewa katika mchakato mzima.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Joseph Warioba alisema tume yake itaondoa mawazo yote hasi yanayokinzana na misingi ya kitaifa.

Jaji Warioba, alisema ni dhamira yake kutengeneza Katiba inayokidhi maslahi ya wananchi wenyewe, lakini pia Katiba yenye kuzingatia misingi na maslahi ya taifa.

Alitaja baadhi ya mawazo yanayokinzana na misingi ya kitaifa kuwa ni pamoja na yale yanayohusu muungano, Serikali ya majimbo, madaraka ya Rais na kinga za wabunge.

Alisema kimsingi tume yake, italazimika kuingilia mawazo ya aina hiyo na kufanya uamuzi mgumu, ili kulinda maadili na maslahi ya kitaifa.

“Katika hili naomba Watanzania watuelewe masuala haya tutayatolea uamuzi. Kama mnavyojua watu wengine walitaka Muungano wa Serikali mbili, wengine walitaka muungano wa Serikali tatu, wengine muungano wa mkataba na wengine walitaka visiwa vya Pemba na Unguja vijitenge. 

“Wengine walitaka Serikali za majimbo, wengine walizungumzia madaraka ya rais na kinga za wabunge ziondolewe, sasa masuala yanayokinzana kama haya lazima tutayatolea maamuzi magumu ili tupate muafaka.

“Lakini pia kuna baadhi ya maoni mengine tutayaacha ingawa yalijadiliwa na wananchi, tunachowaomba Watanzania wawe tayari kuyajadili kwenye rasimu itakayoletwa mbele yao.

“Kama kila kikundi kitataka mawazo yake yaingie kwenye rasimu hatutafikia muafaka, katika masuala ya msingi tutayachagua baadhi ya mawazo na mengine tutayaacha,” alisema Warioba.

Kuhusu kuvurugwa kwa uchaguzi wa mabaraza ya Katiba, Jaji Warioba alivitupia lawama vyama vya siasa na makundi ya kidini na kusema kwamba wanahusika moja kwa moja kuvuruga mchakato huo.

Hata hivyo Jaji Warioba alisema licha ya kujitokeza kwa kasoro hizo, lakini tume yake inasonga mbele kwa madai kuwa kurudia ni kuchelewesha upatikanaji wa Katiba mpya.

Alisema ni kweli uchaguzi huo ulikuwa na matatizo, lakini pale ambapo uchaguzi haukufanyika hali ilichangiwa na mivutano ya kisiasa na ile ya kidini.

“Katika baadhi ya maeneo mikutano ya uchaguzi ngazi za vijiji, mitaa na shehia ilishindwa kufanyika kutokana na mivutano ya kisiasa na kidini, wananchi walifungamanisha chaguzi hizo na masuala hayo.

“Tume tumesikitishwa na namna watu walivyojihusisha pia na vitendo vya rushwa, hivi mtu unahonga katika mabaraza ili iweje, hivi Tanzania tunakwenda wapi?,” Alihoji.

Warioba alisema, uchaguzi wa mabaraza umefanikiwa kwani viongozi na watendaji katika ngazi za vijiji, mitaa, shehia na kata walizingatia mwongozo uliotolewa na Tume na maeneo mengi wananchi walichaguana kwa amani.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, shehia 323 sawa na asilimia 96.4 kati ya shehia 335 kwa upande wa Zanzibar zimekamilisha vizuri mchakato huo, ambapo kata 3,331 kati ya kata 3339 sawa na asilimia 99.8 kwa Tanzania Bara zimekamilisha mchakato wa kuwapata wajumbe wa mabaraza ya Katiba ngazi ya wilaya.

Kuhusu kulalamikiwa kwa watendaji wa kata kuchakachua majina ya wagombea ambao walishinda katika ngazi za vijiji na mitaa, Warioba alishangaa kupingwa uongozi ambao tayari unatumika kuchagua viongozi.

“Wote tunajua uongozi wa WDC ndiyo mara zote unachagua kamati za maji, shule, afya, barabara na nyinginezo, lakini uongozi huo usiaminiwe wakati wa uchaguzi wa mabaraza ya Katiba.

“Sheria za Serikali za mitaa sura ya 287 na 288 Mamlaka za wilaya na miji, zinaelekeza kata kuwa na vikao vya kamati za maendeleo za kata kwa Tanzania bara. 

“Vikao hivyo hushirikisha madiwani wote wakiwemo wa viti maalum wa kata husika, wenyeviti wa vijiji/mitaa na kata husika, hawa ndio wanaoruhusiwa kupiga kura kwenye maamuzi yoyote katika kikao hicho,” alisema.

Kuhusu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kutishia kujitoa katika mchakato huo iwapo Tume yake itashindwa kurekebisha kasoro zilizojitokeza, alisema:

“Sisi tutapeleka rasimu kwa kila mdau, hao wanaotaka kujitoa mimi sitaki malumbano na wanasiasa, nadhani tume haitengenezi Katiba ya vikundi bali ya wananchi,” alisema.

Jaji Warioba alisema Tume yake itaunda na kusimamia mabaraza ya watu wenye ulemavu, ili kuwapa fursa watu hao bara na visiwani kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba.

Alisema Baraza moja litaundwa Tanzania bara na jingine Zanzibar na kwamba yatashirikisha wananchi kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa.

BABA MZAZI BONGO AMNGILIA MTOTO WAKE WA KIKE !!!


Morogoro. Polisi mkoani Morogoro wanamshikilia mkazi wa mjini hapa kwa tuhuma za kumbaka na kumsababishia maumivu makali mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka minane mwanafunzi wa darasa la kwanza.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa, John Laswai alisema kuwa tarehe na muda usiofahamika mwanaume huyo kwa muda mrefu alikuwa akimwingilia kimwili mtoto wake huyo anayesoma katika shule ya msingi.
Laswai alisema kuwa mwanaume huyo siku ya tukio alimwingilia mtoto wake, lakini kabla ya kufanya kitendo hicho alimtuma mtoto wake wa kiume ambaye ni bubu mwenye umri wa miaka 13 dukani mtoto huyo aliporudi alikuta baba yake akitaka kumfanyia unyama huo mdogo wake ndipo alimsadia na wakati wakitaka kukimbia baba alimshika mtoto wa kike na kumfungia ndani.
Kaimu kamanda huyo alisema kuwa baada ya mtoto wa kiume kuona mdogo wake kafungiwa ndipo alipotoa taarifa kwa majirani na kwenda polisi kutoa taarifa,baada ya polisi kufika walimkuta baba huyo akimbaka mwanaye huyo huku akiwa amempiga na kumchoma moto sehemu za usoni.
Alisema kuwa baba huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya uchunguzi kukamilika na kwamba mtoto kwa sasa yuko katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.
Mtoto huyo akizungumza kwa taabu namna ilivyokuwa alisema kuwa baba yake amekuwa akimfanyika kitendo hicho mara kwa mara na anapokataa huwa anampiga na kumtishia kumuua na aliongeza kuwa yeye na kaka yake wamekuwa wakiishi katika hali ya mateso kutoka kwa baba yao na kwamba mama yao aliachana na baba huyo na yuko mkoani Singida
Kwa upande wake Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Grace Massawe akizungumza hospitalini hapo alikiri kumpokea mtoto huyo huku akiwa katika maumivu na majeraha sehemu za usoni.

AL-ALJAZEERA YAFUNGIWA IRAQ !!!


Seriakli ya Iraq imekifungia kituo cha televisheni cha kimataifa cha Aljazeera na vituo vingine tisa vya nchini humo siku ya Jumapili, baada ya kivituhumu kwa kuchochea vurugu za kidini.
Hatua hii imemulika wasiwasi unaozidi wa serikali inayoongozwa na washia, juu ya hali ya usalama inayozidi kudorora, wakati wa machafuko ya waumini wa kisunni na makabiliano yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 180 katika muda wa chini ya wiki moja. Kusimamishwa kwa vituo hivyo ambako utekelezaji wake ulianza mara moja kunaonekana kuvilenga hasa vituo vya kisunii vinavyojulikana kwa kuikosoa serikali ya waziri mkuu Nouri al-Malik.
Wanamgambo wenye silaha wanaoipinga serikali kutoka maeneo ya wasunni wakiandamana mjini Ramadi, mashariki mwa Baghdad.Wanamgambo wenye silaha wanaoipinga serikali kutoka maeneo ya wasunni wakiandamana mjini Ramadi, mashariki mwa Baghdad.
Pamoja na kituo cha Aljazeera, uamuzi huo uliviathiri vituo nane vya kisunni na kimoja cha kishia. hatua hii ya serikali imekuja huku utawala mjini Baghdad ukijaribu kukabiliana na ongezeko la machafuko nchini humo, yaliyoripuka siku chache zilizopita, baada ya vikosi vya usalama kuanzisha operesheni ya ukandamizaji dhidi ya kambi ya waandamanaji wa kisunni katika mji wa kati wa Hawija, na kuua watu 23, wakiwemo wanajeshi watatu.
Tangu wakati huo, zaidi ya watu 180 wameuawa katika mapigano na vikosi vya usalama na mashambulizi mengine. Wimbi la hivi karibuni la vurugu linafuatia miezi minne ya maandamano ya amani ya waislamu wa madhehebu ya sunni, dhidi ya serikali ya waziri mkuu Nouri al-Maliki. Watazamaji nchini Iraq watanedelea kutizama vituo hiyvo, lakini tangazo la kusitishwa kwake lililotolewa na tume ya mawasiliano na vyombo vya habari linasema kama vituo hivyo kumi vitajaribu kuendesha shughuli zake katika ardhi ya Iraq, vitakabiliwa na hatua za kisheria kutoka kwa vyombo vya usalama. Kimsingi amri hiyo inawazuia wanahabari kutoka vituo hivyo kufanya kazi zao nchini Iraq.
Aljazeera yashtushwa na kufungiwa
Mbunge wa Kisunni Dahfir al-Ani aliielezea hatua hiyo kama sehemu ya majaribio ya serikali kuficha umuagaji damu uliyofanyika mjini Hawija na kile kinachoendelea katika maeneo mengine nchini humo. Al-jazeera ilisema katika taarifa kuwa imeshangazwa na hatua hiyo ya serikali ya Iraq, na kuongeza kuwa imekuwa ikiripoti pande zote za habari nchini Iraq kwa miaka mingi. Aljazeera iliripoti kwa undani kuhusu mapinduzi katika mataifa ya kiarabu, na imekuwa ikiripoti kwa kiasi kikubwa kuhusu mgogoro unaondelea nchini Syria.
Magazeti na vyombo vingine vya habari vilianzishwa nchini Iraq baada ya kuanguka kwa utawala wa Saddam Hussein mwaka 2003, lakini nchi hiyo imeendelea kuwa mmoja yenye hatari zaidi kwa waandishi wa habari, ambapo zaidi ya 150 wameuawa tangu mwaka 1992, kwa mujibu wa kamati ya kulinda waandishi wa habari.
Waziri Mkuu wa Iraq Nouri al-Maliki.Waziri Mkuu wa Iraq Nouri al-Maliki.
Iraq na serikali nyingine za mashariki ya kati ziliwahi kufunga ofisi za Al-Jazeera kwa muda huko nyuma, kwa sababu hazikupendezwa na jinsi inavyoripoti matukio. Vituo vingine tisa ambavyo leseni zake zimefungiwa na tume ya mawasiliano ya Iraq ni pamoja Al-Sharqiya na Al-Sharqiya News, ambacho kinaikosoa serikali mara kwa mara, na vituo vingine vidogo saba vikiwemo Salahuddin, Fallujah, Taghyeer, Baghdad, Babiliya, Anwar 2 na al-Gharbiya.
Televisheni ya Baghdad yasema ni uamuzi wa kisiasa
Televisheni ya Baghdad iliyopo mjini Baghdad, ilisema uamuzi huo ulikuwa ni wa kisisiasa. "Serikali ya Iraq haina uvumilivu kwa maoni yanayokinzana na wanajaribu kunyamanzisha sauti zinazokwenda kinyume na msismamo rasmi," alisema Omar Subhi, mkurugenzi wa kitengo cha habari. Alisema Televisheni hiyo ilikuwa na wasiwasi juu ya usalama wa wafanyakazi wake, ikihofia kuwa vikosi vya usalama vinaweza kuwafukuza.
Katika taarifa iliyochapishwa katika mtandao wake, tume ya habari ya serikali ilivilaumu vituo vilivyofungiwa kwa kuongezeka kwa wasiwasi wa kidini, ambao unachochea vurugu zilizofuatia mapigano ya maafa mjini Hawija. Tume hiyo ilivishtumu vituo kwa kutoa ripoti za upotoshaji na zilizotiwa chumvi, kutangaza wito wa dhahiri wa uvunjivu wa amani, na kuanzisha mashambulizi ya kihalifu ya kulipiza kisasi dhidi ya vyombo vya usalama. Pia ilivilaumu vyombo hivyo kuyatangaza makundi ya kigaidi yaliyopigwa marufuku, yaliyotenda uhalifu dhidi ya watu wa Iraq.
Osama Abdul-Rahman, mfanyakazi wa serikali wa madhehebu ya kisunni kutoka kaskazini mwa Baghdad, alisema serikali inatumia sera ya ndumila kuwili kuhusiana na vyombo vya habari, kwa kuvifumbia macho vituo kadhaa vya kishia ambavyo anadai vinachochea vurugu. "Vituo vilivyo karibu na vyama vikuu vya kishia na hata televisheni ya taifa pia vinarusha vipindi vya ubaguzi wa kidini vinavyochochea vurugu muda wote, lakini hakuna mtu anaevisimamisha," aliongeza.
Wananchi wakibeba jeneza la mwanajeshi alieuwawa katika vurugu za hivi karibuni.Wananchi wakibeba jeneza la mwanajeshi alieuwawa katika vurugu za hivi karibuni.
HRW yasema madai ya serikali yana mashaka
Erin Evers, mtafiti wa masuala ya mashariki ya kati kutoka shirika la haki za binaadamu la Human Rights Watch, aliyaita madai ya serikali kwamba imevivhukuliwa hatua vituo vya televisheni kwa kuchochea ubaguzi wa kidini kuwa ya mashaka, kwa kuzingatia "historia yake endelevu ya ukandamizaji dhidi ya vyombo vya habari - hasa vyombo vya habari vinavyoegemea upinzani -hasa katika nyakati nyeti kisiasa."
"Kufungiwa kwa vituo hivyo ni ushahidi mwingine kuwa serikali inataka kuzuia kuripotiwa kwa habari wasizozipenda," alisema Evers. Aliituhumu tume ya habari ya Iraq kwa kuchanganya ripoti ya hotuba iliyo na vidokezo vya ubaguzi wa kidini na kuchochea kwa wazi kwa vurugu za kidini. "Haya ni mambo mawili tofauti kabisaa na lwa kwanza linalindwa chini ya sheria za kimataifa na za Iraq pia," alisema.
Uamuzi wa kufungia vituo hivyo ulikuwa wakati ambapo al-Maliki akihudhuria isivyo kawaida katika maziko rasmi ya wanajeshi watano waliouawa siku ya Jumamosi, na watu wenye silaha katika mkoa wa wasunni wa Anbar. Polisi katika mkoa huo ilisema wanajeshi hao waliuawa katika mapigano baada ya gari lao kusimamishwa karibu na kambi ya maandamano ya wasunni.
Matukio ya mashambulizi kama hili yameongezeka nchini Iraq.Matukio ya mashambulizi kama hili yameongezeka nchini Iraq.
Serikali ilitoa muda wa masaa 24 kwa waandaji wa maandamano hayo kukabidhi watu waliohusika na mauaji hayo, au wakabiliwe na hatua kali. Lakini hakuna mtu aliekabidhiwa na muda uliyotolewa umepita. Siku ya Jumamosi, watu wenye silaha wakitumia bunduki zilizofungiwa vifaa vya kuzuia sauti, walipiga risasi na kuwauwa viongozi wawili wa kikabila wasunni katika matukio mawili tofauti ya kusini mwa Baghdad.
Miripuko yazidi kutikisa
Wakati huo huo, miripuko mitatu ya mabomu yaliyotegwa kwenye magari imesababisha vifo vya watu wasiopungua 20 kusini mwa Iraq siku ya Jumatatu, katika maeneo yanayokaliwa na washia wengi. Mripuko moja ulitokea karibu na soko, wakati mwingine ulitokea karibu na mkusanyiko wa wafanyakazi katika mji wa Amara, uliyopo kilomita 400 kusini-mashariki mwa Baghdad. Mripuko huo uliua watu 16 na kujeruhi 25.
Kkatika mji wa Diwaniya, uliyoko kilomita 150 kusini-magharibi mwa Baghdad, bomu la kwenye gari liliripuka karibu na mgahawa, na kuua watu wanne na kujeruhi wengine 11. Kuongezeka kwa vurugu hizi kunaongeza hofu ya kurudisha vurugu za kidini zilizoipeleka nchi hiyo karibu na kuripuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya mwaka 2006 na 2007.

Monday 29 April 2013

PADRI AFUMANIWA LIVE AKILA URODA NA MKE WA MTU !!!


Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi limeingia katika kashfa nzito baada ya padri wake, Father Urbanus Ngowi wa moja ya parokia zake kudaiwa kufumaniwa na mwanamke anayesemekana ni mke wa mtu.
Sakata la fumanizi hilo linadaiwa kutokea Jumatatu ya wiki iliyopita chumbani kwa padri huyo, Marangu Wilaya ya Moshi Vijijini ambako Father Ngowi inasemekana alikutwa ‘laivu’ akiwa na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.
Pamoja na kunaswa huko, vyanzo havijaeleza humo chumbani wawili hao walikuwa wakifanya nini!
Habari zinadai siku ya tukio, mwanamke huyo aliingia nyumbani kwa padri huyo ambapo baadhi ya ndugu wa mumewe walikuwa wakimfuatilia baada ya madai yaliyokuwepo kwamba ana ukaribu wenye maswali mengi na mtumishi huyo wa Mungu.
“Unajua siku nyingi ilivuma kwamba Mama P na Father Ngowi wana ukaribu wenye maswali mengi, mume wake alifuatilia na kubaini ni kweli lakini akashindwa kuutenganisha ukaribu wao,” kilidai chanzo.
Chanzo kikaendelea kudai kwamba baada ya kuona mkewe amejikita kwa mtumishi wa Mungu, mumewe alinyoosha mikono juu na kumwachia Mungu.
Chanzo: Sasa siku hiyo baada ya ndugu wa mume kumfuatilia mpaka anaingia kwa Father Ngowi, wakaona ni bora watafute mpigapicha ili kupata picha za tukio ambazo zitakuwa ushahidi siku za mbele.
“Walipompata wakazama ndani, sekeseke likaanzia hapo. Walimkuta mwanamke huyo na mtumishi wa Mungu wapo kitandani.”
Habari zinadai kwamba kufuatia tukio hilo, tayari Kanisa Katoliki limemweka kitimoto padri huyo ambaye alikuwa akihudumu katika Parokia ya Korongoni, Moshi Vijijini kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Parokia ya Makomu, Marangu ambako inadaiwa ameshushwa cheo.
Inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo, Father Ngowi alikana kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake lakini alipobanwa sana na mabosi wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Moshi, alikiri na kudai ibilisi alimpitia na kuomba kanisa limsamehe na kutompa adhabu kali ambayo itamuathiri kisaikolojia.
Hili ni tukio kubwa na la aina yake kuwahi kulikumba Kanisa Katoliki nchini kwa padri wake kudaiwa kukutwa na mke wa mtu chumbani
Kuna madai kwamba mwaka jana (2012), Father Ngowi, mbele ya waumini wake alisoma barua yenye kukana shutuma zote zilizoelekezwa kwake kwamba amekuwa na ukaribu wenye maswali mengi na wake za watu.
Taarifa zilidai kuwa padri huyo aliweka wazi akisema si kweli kwamba amekuwa na ukaribu unaotajwa, akawataka waumini wake wapuuze tuhuma hizo alizosema zina mwelekeo wa kuchafua sifa yake na taswira ya Kanisa Katoliki kwa jumla.
Hayo ni madai ya vyanzo vyetu ambavyo viliambatanisha na picha mbalimbali za tukio hilo lenye kushtua waumini sambamba na namba za simu za padri huyo kwa ajili ya mawasiliano ili kujiridhisha.

Sunday 28 April 2013

MSHUKIWA WA MABOMU YA BOSTON AHAMISHIWA JELA!!!


Maafisa wa Marekani wanasema mshukiwa wa mabomu yaliyolipuliwa wakati
wa Boston Marathon,  Dzhokar Tsarnaev amehamishiwa kwenye kituo cha afya katika jela ya  serikali kuu kutoka hospitali ambapo alikuwa akipata matibabu kwa majeraha aliyopata wakati alipokamatwa wiki iliyopita.

Idara ya usalama ya Marekani ilisema Ijumaa kwamba Tsarnaev  alihamishiwa kwenye kituo cha afya cha  serikali kuu  cha Devens kwenye eneo la  kituo cha jeshi huko Fort  Devens, katika jimbo la Massachusets.

Msemaji hakutoa taarifa juu ya hali ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 19, ambapo maafisa wamesema anapata matibabu ya jeraha lake la shingo. Idara ya magereza imesema eneo la Devens ni jela ambayo   inatoa  matibabu ya hali ya juu au ya muda mrefu kwa wafungwa.

Kaka wa mshukiwa na mshiriki  katika ulipuaji mabomu,Tamela Tsarnaev alifariki katika mapigano na Polisi usiku wa alhamisi wiki iliyopita.

Maafisa wa New York wanasema washukiwa hao walikuwa wakipanga mashambulizi huko Times Square wakati wakikimbia maafisa. Mkuu wa Polisi wa New York Ray Kelly  anasema Dzokhar aliwaambia wachunguzi walipanga waende  New York ili kulipua milipuko yao iliyobaki.

Friday 26 April 2013

KWA NIONAVYO MIMI !!! SEREKALI YA TANGANYIKA NA UDINI !!!

Kwa nionavyo mimi: ila kubwa ambalo waislamu wamekua wakilalamikia ni upendeleo wa serikali kwa wakristu huku ikiwaacha waislamu. angalieni mifano ifuatayo;
1- waislamu wamekua wakilalamikia serikali kutotambua siku ya ijumaa kama siku ya ibada. wakristo wana jumapili lkn waislamu waliyo wengi wamekua wakishindwa kufanya ibada kutokana na ijumaa kuwa siku ya kazi. wameomba pia kama inawezekana angalau saa 5 na nusu hadi saa nane uwe muda rasmi wa kuwaruhusu waislamu kwenda kufanya ibada siku za ijumaa. la ajabu hadi bunge huendelea na mijadala mida ya adhuhuri siku za ijumaa.
2- waislamu wamekua wakilalamikia upendeleo uliyofanywa na serikali kwa kuingia mkataba na TEC na CCT. mkataba huo unajulikana kama MEMORANDUM OF UNDERSTANDING. waislamu wanajiona kama mtoto ambaye anawekwa kando huku kaka yake akiendelezwa kwa kupewa mtaji wa biashara.
3- waislamu wamekua wakilalamikia kutopata fursa ya kuwa na mahakama za kadhi zinazotambulika rasmi kikatiba. wamefafanua kuwa mahakama a kadhi itahusu mirathi, ndoa, talaka na wakfu. mambo ya jinai hayamo kwenye mahakama ya kadhi. licha ya mambo haya kuwa IBADA kwa waislamu, wakristo wamekataa katakata uanzishwaji wa mahakama ya kadhi. waislamu kwa upande wao wameona kuwa wanaingiliwa katika ibada yao. wametoa mifano kuwa uganda. afrika ya kusini, uingereza nk... kuna mahakama za kadhi licha ya hizi nchi kuwa na idadi ndogo za waislamu.
4- waislamu waliwahi kushauri nchi yetu ijiunge na oic. walieleza faida za kujiunga na oic kiuchumi. wakristo wakamekataa suala la oic. wanasema nchi haina dini. haiwezi kusajiliwa kuwa ya kiislamu. uganda, msumbiji nk... ni wanachama wa oic.
5- waislamu wamelalamikia NECTA kuwa na viongozi wakristo watupu. hakuna muislamu pale. muislamu kama yupo atakua mfagiaji. mwaka juzi na jana, ilibainika kuwa watoto wa kiislamu walifelishwa mtihani wa islamic knowledge. NECTA walikira na kusema kuwa ni kosa la kikompyuta. hakuna akiejiuzulu!
6- waislamu wamelalamikia kuwekwa kando katika ajira ya umma. wanasema kuwa wakristo ni wengi maofisini. wanaendelea kubebana licha ya kuwepo waislamu wenye sifa. baadhi ya ofisi za serikali zinaonekana kama parokia. wameombwa pawe na mpango mkakati wa kuwachomeka kwenye ajira serikalini (wenye sifa) ili angalau nao washiriki katika matunda ya keki ya taifa.
7- waislamu wanasema wamekua kwa miaka mingi wakichukuliwa kama minority group. ktika sensa ya mwaka jana, waliomba kiwekwe kipengela cha sensa ili ukweli wa idadi ya watu kidini ujulikane. walitoa mfano kuwa inasemekana wakristo ni wengi. hivyo, inapopangwa mipango ya maendeleo kwa mfano ardhi kwa ajili ya nyumba za ibada na maziko, wakristo hupewa maeneo makubwa kwa madai kuwa ni wengi.
8- waislamu wamekuwa wakilalamika kuwa nchi yetu inaendeshwa kwa mfumo kristo. wanasema kipindi cha sikukuu, ofisi za serikali hupambwa muda wa sikukuu za wakristo. sikukuu za waislamu hakuna kinachofanyika!
9- kama ulivyo sema, waislamu wanalalamika kuwa serikali imekua ikiikumbatia sana BAKWATA na kudharau taasisi nyingine za kiislamu. BARAZA KUU ni taasisi yenye waislamu wengi hapa nchini kuliko bakwata. serikali huwa haiipi taasisi ya baraza kuu uzito wowote.
UFAHAMU WANGU :
kundi katika jamii linaposononeka kwa muda mrefu, hukata tamaa. baada ya kukata tamaa kupoteza imani na serikali yao. waislamu wanaamini kuna urafiki mkubwa kati ya serikali na ukristo. hali hii inawafanya wawachukie wakristo wakiwaona kuwa wabaya wao. hoja ya kusema rais, makamu, rais na wakamu wawili wa znz, igp, jaji mkuu kuwa wote ni waislamu haina mashiko. hawa siyo watendaji mkoa, wilaya, kata hadi kijiji. mfumo wanasema ni wakikiristo. hata kama viongozi wa juu watakua waislamu, hilo ni kiini mamcho.

nashauri upande wa wakristo watambue na kutafakari madai ya waislamu kuliko kuwadhihaki kuwa "wala ubwabwa hao, wavaa kanzu hao, wavaa msuli hao..........". kuwadhihaki ni kungeza mpasuka ambao unafanya amani na umoja vizidi kutoweka.

SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR !!!


Ndege za kivita zikiwa hewani zikifanya shoo katika sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Ndege hizi ni za Muungano wa Tananyika na Zanzibar, Wazanzibar tukivunja Muungano tunagawana nusu kwa nusu ,hakuna mkumbwa wala mdogo ,viongozi hilo lazima mlijuwee, nawakilisha

Thursday 25 April 2013

HOW HIGH ? MOMBASA'S DRUG MENACE!!!


CCM OYEEE , CCM OYEEE, CCM OYEEE

Vijana wa Tawi la CCM Bweleo wakimshangila Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar 

MAANDAMANO LONDON MBELE YA UBALOZI WA SAUDIA !!!



Maandamano London mbele ya ubalozi wa Saudia
Makumi ya watu mbalimbali wakiwemo Waislamu waishio nchini Uingereza, wamefanya maandamano mbele ya ubalozi wa Saudi Arabia wakipinga hakumu ya kutaka kunyongwa mwanazuoni wa Saudia sheikh Nimr Baqir al-Nimr. Maandamano hayo yamefanyika leo mjini London, Uingereza. Katika maandamano hayo yaliyowashirikisha Waislamu wa Bahrain, Saudi Arabia, India, Pakistan na Iraq, waandamanaji walitoa nara za kulaani utawala wa Aal Saudi, kuwa ni muenezaji wa ugaidi duniani. Aidha waandamanaji wamesisitiza juu ya kukomeshwa uingiliaji wa masuala ya ndani ya Bahrain sambamba na kutaka kuachiliwa huru mwanazuoni huyo anayeendelea kuzuiliwa katika korokoro za Aal Saudi. Aidha waandamanaji hao waliokuwa wamebeba mabango mbalimbali, wamelaani vikali uungaji mkono wa Rais Barack Obama wa Marekani kwa utawala wa Saudia. Katika maandamano hayo Said al-Shahabi, Mkuu wa Kituo cha Tamaduni mjini London amesema kuwa, maisha ya Sheikh Nimr Baqir al-Nimr yako hatarini na kwamba, Marekani na Uingereza kwa kuziunga mkono tawala za Bahrain za Saudia zinahusika moja kwa moja katika umwagaji damu wa raia wasio na hatia  na wapigania uhuru duniani.

WAISLAM WAZUIWA KUJENGA MSIKITI FRANCE !!!



Msikiti Mkuu katika mji mkuu wa Ufaransa, ParisMsikiti Mkuu katika mji mkuu wa Ufaransa, Paris
Waislamu wa mji wa Montrouge nchini Ufaransa wamepanga kufanya maandamano makubwa ya kulalamikia hatua ya manispaa ya mji huo ya kupinga kujengwa msikiti mjini humo. Kituo cha habari ya Echo-Montrouge kimewataka Waislamu wa mji wa Montrouge wa kusini mwa mji mkuu wa Ufaransa, Paris, kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano hayo ili kulalamikia hatua ya manispaa ya mji huo ya kuzuia kujengwa kituo pekee cha ibada kwa Waislamu mjini humo. Maandamano hayo yamepangwa kufanyika wiki ijayo yaani Aprili 27, na mkuu wa Jamii ya Waislamu wa Ufaransa, Nabil an Nasri, na mkuu wa jamii ya kupambana na chuki dhidi ya Uislamu, Sami Dabbah, watahutubia waandamanaji na kusisitiza juu ya haki ya Waislamu wa mji huo ya kuwa na msikiti. Jumuiya ya Kudumisha Udugu ya mji wa Montrouge ndiyo iliyoitisha maandamano hayo na imewataka wananchi wote wa Ufaransa kushiriki kwenye maandamano hayo. Ujenzi wa msikiti katika mji wa Montrouge huko Ufaransa ulianza miaka minne iliyopita lakini miezi miwili tu tangu kuanza ujenzi huo, manispaa ya mji huo iliingilia kati na kuzuia kuendelea kujengwa sehemu hiyo ya ibada kwa Waislamu. Waislamu wa Ufaransa walipigania sana haki yao hiyo na mwaka huu wa 2013 wamepewa tena kibali ya kuendelea kujenga msikiti huo lakini hivi sasa pia manispaa ya mji wa Montrouge imeingilia tena kati na kuzuia ujenzi huo kwa madai kuwa Waislamu mjini humo ni wachache hivyo hawana haki ya kuwa na msikiti.

AIBU: MKE WA MTU ANASWA LIVE AKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI MAENEO YA MWENGE-DAR

KUFUATIA vitendo vya usaliti wa ndoa, uasherati, ufuska na ukiukwaji wa maadili ya Kitanzania kwa wanandoa, wiki iliyopita Ijumaa iliendelea na Operesheni Fichua Maovu kwa kuzunguka jijini Dar usiku wa manane na kunasa tukio la mke wa mtu akifanya uzinzi ndani ya gari. 


Kabla ya kufanya operesheni hiyo, waandishi  walitaarifiwa kwamba Wilaya ya Kinondoni jijini Dar ndiyo inayoongoza kwa wake na waume  za watu kufanya vitendo vya ngono kwenye magari.
 
Maeneo yaliyodaiwa kwamba wazinzi hao hupenda kuyatumia ni Coco Beach, Leaders Club, Mlimani City na sehemu kubwa ya vitongoji vya Sinza na Mwenge, Dar.

Mbali na waume na wake za watu, wengine wanaotajwa kufanya vitendo vya ngono ndani ya magari ni mastaa wakubwa ambao wanaogopa kwenda kukodi vyumba mahotelini na gesti wakihofia watajulikana kutokana na umaarufu wao.Jumatatu ya Aprili Mosi, mwaka huu, waandishi wetu walianza mchakato wa kutembelea vitongoji walivyoezwa kwamba, watu hususan wake na waume za watu hupenda kuvitumia kufanyia ufuska.Waandishi wetu walitinga kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay, Dar ambako walishuhudia wasichana wengi waliokuwa wakifanya biashara ya kujiuza ‘machangudoa’ katika viunga hivyo.

Mbali na wasichana hao, pia kulikuwa na vibaka wengi waliokuwa wakiwalinda machangudoa hao ili wasipate matatizo.

Pia, wanaume wengi walikuwa wakifika na wanawake ndani ya magari yao na kupozi kwenye maegesho, wengi wao hawakuonekana kama ni watu na wake zao.

 Hata hivyo, waandishi walibaini kwamba magari mengi yanayotumiwa katika eneo hilo ni yale yenye vyoo vyeusi ‘tinted’ hivyo ni vigumu kujua kinachoendelea ndani yake.

Kwa ujanja, waandishi wetu walibaini kwamba ‘pea’ nyingine zilikuwa zikifanya vitendo vya ‘kudendeka’ na wengine kufika mbali zaidi lakini walishindwa kuwavaa kutokana na usalama mdogo katika eneo hilo.


Waandishi  wetu walihamishia mtego wake Leaders Club, Kinondoni mida ya saa 8:05, baada ya kupiga misele ya hapa na waandishi walifanikiwa kumbamba mmoja wa wazinzi.

Waandishi walitulia baada ya kuliona gari aina ya Toyota Land Cruiser  likiwa katika eneo la maficho nje ya viwanja hivyo.

Gari hilo lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba mchezo ulikuwa ukiendelea ndani yake.

Wakati waandishi wakijipanga kulivamia, ghafla waliokuwa ndani walishtuka na kupozi kwa muda.

Hata walipoachiwa ili waendelee, machale yaliwacheza na kuwasha gari kisha kuondoka kwa kasi.


Pamoja na kulikosakosa tukio hilo, waandishi hawakukata tamaa, kuanzia Jumatatu hadi Jumapili waliendelea na utaratibu wa kutembelea viwanja husika.

Jumapili iliyopita baada ya kutembelea viwanja vyote kusaka ‘wahalifu hao’, hatimaye mtego ulinasa.


‘Patroo’ ikiwa kazini maeneo ya Mwenge, Dar jirani kabisa na hoteli moja inayopata umaarufu mkubwa siku za hivi karibu, ghafla gari aina ya Toyota Corona likiwa limepaki kwenye eneo la giza, chini ya mti lilikuwa likitikisika kuonesha kwamba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya ngono

TAWHEED SUNNAH MALI !!!

Mujaahidina wa Mali (Ansaru Dini) Leo wamemchinja Askari moja kutoka Chad baada ya kukamatwa akiwa hai, inasemikani huyu askari alikamatwa baada ya kuishiwa risasi na baadhi ya wenzake walikufa kwenye Mapambano. ALLAHU AKBAR.

KUZUMZUNGUMZIA MUUNGANO KOSA ?MBONA MWENGINE WAPO NDANI ???

GARIMOSHI la Katiba mpya linaendelea kwenda kasi na hakuna dalili ya kukoma mpaka Katiba “mpya” itakapopatikana.

Msisitizo hadi sasa umekuwa juu ya ujio wa “Katiba mpya” hata kama upya wake utakuwa bado na mambo ya zamani. Mchakato huu ambao ulikosewa toka mwanzo una kila dalili ya kufanya zoezi la Katiba mpya kutofanikiwa na kutokukidhi mahitaji ya Watanzania.

Sheria inayosimamia mchakato huu na ambayo iliweka uwezekano wa tume ya Katiba kuundwa imeweka wazi mambo kadhaa ambayo wananchi (yaani wenye nchi) hawapaswi kuyazungumzia na kuyabadilisha isipokuwa tu kujadili kwa namna ya kuboresha. Yaani, wananchi (wenye nchi) wakitaka kuondoa jambo fulani kati ya haya, sheria inakataza.

Kifungu cha 9 cha Sheria hiyo ya 2011 kifungu kidogo cha 2 kimeweka orodha ya mambo ambayo ni lazima yadumishwe kwenye Katiba mpya na la kwanza kati ya hayo ni “kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano”.

Jambo hili kwa haraka laweza kuonekana kuwa ni jema, lakini tukiangalia kwa karibu tutaona kuwa kwa maamuzi ya watu walioko madarakani mojawapo ya matatizo makubwa kabisa ya kisiasa ambalo Taifa linahangaika nalo ni hili – uwepo wa Jamhuri ya Muungano.

Ikumbukwe kuwa tulipoungana na kuunda taifa la Tanzania tulikuwa nchi mbili kila moja ikiwa na hakimiya kamili. Kulikuwa na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kulikuwa na Jamhuri ya Tanganyika. Nchi hizi mbili ziliungana na kuunda nchi hii ya Tanzania. Tangu wakati huo hadi sasa hata hivyo Muungano wetu umekuwa sababu ya fahari lakini pia sababu ya maswali.

Miaka ya karibuni maswali haya yameanza kugeuka na kuwa shari baina ya watu wa pande zetu mbili. Kuna mgogoro ambao tayari umehusisha viongozi wa kitaifa. Wapo wananchi wa Zanzibar ambao wanaamini kuwa pamoja na kuingia katika Muungano, Zanzibar ilibakia kuwa nchi na imeendelea kuwa nchi. Hawa wanachodai ni kuwa kilichopotea baada ya Muungano ni serikali ya Tanganyika lakini Zanzibar imeendelea kuwapo.

Matokeo yake ni kuwa Wazanzibari wameendelea kushikilia Zanzibar lakini wakati huo huo wanadai Tanzania. Wazanzibar wana haki zote kama Wazanzibari na wana haki zote kama Watanzania. Wazanzibar wanaweza kuteuliwa katika ajira Zanzibar na wanaweza kuteuliwa katika ajira Bara; wanaweza kuomba kazi Zanzibar wanaweza kuomba kazi Bara; wanaweza kumiliki ardhi Zanzibar na wanaweza kumiliki ardhi Bara. Wazanzibar wakija Bara kwamba wanatoka Zanzibar haichukuliwi kwa namna yoyote tofauti.

Hivyo, Mzanzibari anaweza kwenda Bukoba, Iringa, Mwanza au Tanga na kufanya shughuli zake akijua yuko ndani ya nchi yake. Lakini pamoja na hayo bado ana haki ya kipekee Zanzibar.

Mtu wa Bara (Mtanzania anayetoka Bara) akienda Zanzibar hana haki zile zile isipokuwa kama vile ni mgeni (alien). Hana haki ya ajira au kuteuliwa kwenye nafasi mbalimbali. Rais wa Zanzibar hawezi kumteua mtu wa Bara kufanya kazi za Zanzibar bila kuonekana ameenda ‘nje’ ya Zanzibar kutafuta ajira japo Mzanzibari naye ni Mtanzania na mtu wa Bara naye ni Mtanzania. Mtu wa Bara ni Mtanzania akiwa Tanzania lakini akiwa Zanzibar yeye ni mBara kwani Zanzibar ni ya Wazanzibari lakini Tanzania ni yetu sote.

Mtu wa Bara kwa Zanzibar yeye ni mgeni. Na tumeshuhudia baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakijaribu kutunga sheria zenye kuwashughulikia watu wa Bara kama wageni Zanzibar ndani ya Muungano huu huu.

Inaonekana walioungana ni watu wa Bara lakini watu wa Zanzibar wao bado hawajaungana. Wanataka chetu kiwe cha wote lakini cha kwao kiwe cha kwao. Kisingizio (haiwezi kuwa sababu) ni kuwa ati “Zanzibar ni ndogo”.

Hivyo, kutokana na udogo wake basi ni lazima kuwe na nafasi za kuwalinda Wazanzibari. Hivyo ardhi ni kwa ajili ya Wazanzibar na ajira mbalimmbali ni kwa ajili ya Wazanzibari. Ni sawasawa na kule Marekani ati mtu wa California akienda Michigan aonekane ni mgeni na asiwe na haki hizo japo na yeye ni Mmarekani.

Katika mfumo huu ambao tunaambiwa una kero nyingi mara nyingi kinachoitwa “kero” ni kile ambacho Muungano unaathiri Zanzibar. Lakini maoni yangu ni kuwa kama kuna kero kubwa ya kimfumo ni ile ambayo inawabagua watu wa Bara wanapoenda Zanzibar au wanapotaka kuishi na wao kunufaika na Zanzibar kama sehemu ya nchi yao. Wakati Bara mtu anaweza kutoka Kigoma na kwenda Arusha au kutoka Mwanza kwenda Tabora kujaribu maisha na asipate shida yoyote ya kuonekana mgeni alimradi yeye ni Mtanzania mtu huyo huyo akienda Zanzibar ataonekana mgeni na hatopewa ule ulinzi wa kisheria ambao yeye kama Mtanzania anao katika nchi yake.

Mtu wa Bara anapoenda Zanzibar ni kana kwamba anakwenda nchi nyingine lakini Mzanzibari akija Bara anaenda sehemu ya nchi yake.

Hivyo, swali ambalo huwa watu wanauliza kwanini Wazanzibari wanapewa ajira kwenye wizara zisizo za Muungano lina makosa kwa kiasi chake. Lina makosa kwa sababu Mzanzibari ana haki zote kama Mtanzania lakini si kila Mtanzania ana haki sawa Zanzibar – japo nayo ni Tanzania.

Mzanzibari anapoomba nafasi kwenye chuo kikuu chochote Bara anafanya hivyo kama Mtanzania na nina uhakika Bodi ya Mikopo inatoa mikopo kwa Wazanzibari vilevile – kwa sababu na wao ni Watanzania. Mzanzibari anaweza kuomba kazi kwenye idara au vitengo vya Bara ambavyo si vya Muungano na akapewa ajira hiyo – si kama mgeni (kwa mfano Mkenya au Mganda) bali akapewa nafasi kama Mtanzania kwani hiyo ni haki yake.

Lakini mtu wa Bara hawezi kuomba ajira kwenye idara au kitengo Zanzibar akachukuliwa kama Mtanzania tu; itapaswa ajibu swali kama yeye ni Mzanzibari. Kwani Wazanzibari wana urithi Zanzibar na wana urithi Bara.

Ni katika hili tunaweza kuona kuwa kutozungumzia uwepo wa Jamhuri ya Muungano ni kosa kubwa. Kama Wazanzibari wanataka kuendelea kuwa na nchi yao na ambayo watoto wao watairithi basi wapewe nafasi hiyo. Watu wa Bara nao wapewe nafasi ya kufurahia urithi wao bila watu “wengine” kupewa urithi wasioutaka. Kosa hili la kutokuzungumzia “uwepo wa Muungano” ni kosa ambalo bado litaendelea kutuandama kama jinamizi.

Watu wa Bara nao wataanza kuchoka kuona nafasi “zao” zinachukuliwa na Wazanzibari wakati wao hawawezi kuchukua nafasi kule Zanzibar bila ya kuonekana wanachukua nafasi za “Wazanzibari”.

Hivyo, japo ni kweli wanaweza kutuletea Katiba mpya, hali halisi ni kuwa bado tutakuwa na tatizo lile lile la zamani; Muungano. Hata tukiwa na serikali tatu bado matatizo yatakuwa yale yale.

Je, Wazanzibari watakuwa na haki zozote Tanganyika? Je, Watanganyika watakuwa na haki zozote Zanzibar? Kosa hili litakuja kutugeuka mbele ya safari na kutuumiza kama Taifa. Tufikirie.

KWA NINI UISLAMU UMEHARAMISHA WANAUME KUVAA DHAHABU NA HARIRI?


Leo ulimwenguni kote kutokana na kile kinachojulikana kama wimbi la
kwenda na wakati, uhuru na haki ya mtu kufanya/kuishi atakavyo; si jambo la kushangaza wala kustaajabisha kuwaona vijana wa kiume wakiwa wamejipamba kwa kuvaa mikufu, pete na hata hereni za dhahabu. Hili leo si geni tena bali ni jambo la kawaida na fakhari hata katika miji ya mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, ambako asilimia kubwa ya wakazi wake ni wafuasi wa dini ya Kiislamu kwa miongo ya miaka. Uvaaji huu wa dhahabu kwa vijana wa kiume umeingizwa pande zetu hizi za Afrika ya Mashariki na vijana waliotoka huku kwenda nchi za Ulaya kutafuta ajira hasa ya ubaharia. Hawa waliporejea wakiwa wameuiga utamaduni huo wa kigeni na kuwaathiri vijana wengine, limbukeni wenye kuiga kila kiingiacho mjini.
Utamaduni huu wa vijana wa kiume kujipamba kwa kuvaa dhahabu unakwenda kinyume na utamaduni wa mila ya Kiislamu. Mwenyezi Mungu amemuumba mwanamume na Mwanamke na kumpa kila mmoja maumbile na tabia zinazotofautiana na mwenzake. Ikiwa hili linaashiria kitu, basi si kingine bali ni kutofautiana pia katika nafasi na majukumu ya kila mmoja wao. Nadharia inaonyesha kuwa tabia na maumbile ya mwanaume ni ukakamavu na ugumu, wakati ambapo tabia na maumbile ya kike ni ulaini na ulegevu. Uislamu unamtaka mwanaume alelekee katika mazingira yaliyo mbali na udhaifu,unyonge na anasa zinazoweza kunlegeza ili aweze kuwa imara na mwenye nguvu katika kupambana na harakati za maisha ya kila siku, ambapo sehemu kubwa ya jukumu hilo amebebeshwa yeye na sheria . Sasa kwa kuzingatia kuwa madini ya dhahabu na hariri ni vitu vya anasa ambavyo humfanya mvaaji aonekane amependeza machoni mwake yeye mwenyewe kwanza na machoni mwa wengine na natija yake ni kuvaana na maumbile ya kupendeza ambayo ni ulaini na ulegevu. Pengine kwa njia moja au nyingine hii ndio inaweza kuwa hekima/falsafa ya kuharamishwa dhahabu na hariri kwa wanaume kwa kuwa inakubaliana na tabia na maumbile yao.
Hebu tujaribu kuwa wakweli, tuwatie katika mizani ya haki na uadilifu wanaume wenye kuvaa dhahabu na wasiovaa dhahabu, tutagundua nini? Bila ya shaka mtakubaliana na mimi kuwa ipo tofauti ya dhahiri baina yao, wavaao dhahabu watakuwa wameathirika na tabia na maumbile ya kike. Taathira hii utaiona katika mwendo wao, uzungumzaji wao, uvaaji wao na wakati mwingine huiga hasa tabia za kike kama vile kusuka nywele na kutumia vipodozi.
Ni kweli usiopingika kwamba kujua hekima/falsafa ya kuharamishwa dhahabu na hariri kwa wanaume, hii ni elimu isiyo na manufaa na ni ujinga usiodhuru. Usiulize hekima kwa kuwa kumeshurutishwa katika kuulizia hekima ya amri au makatazo, awe huyo muamrishaji/mkatazaji analingana sawa na kufanana na huyo muamrishaji/mkatazwaji na hapa ni suala la Mungu Muumba Muamrishaji na mwanadamu kiumbe muamrishwa. Kwa mantiki hii mwanadamu hana budi kuikubali na kuipokea amri kwa kuwa Mola wake ameamrisha/amekataza,kisha baada ya kutekeleza aliloamrishwa ndipo anaweza kutafuata kujua hekima/falsafa ya amri ile. Lakini kule kujua hekima/falsafa iliyomo katika amri au katazoisiwe ni sharti ambalo kwanza ni lazima litimizwe kabla ya kuamrika au kukatazika. Muislamu wa kweli anaambiwa na Mola wake:
“HAIWI KWA MWANAUME ALIYEAMINI WALA KWA MWANAMKE ALIYEAMINI, ALLAH NA MTUME WAKE WANAPOKATA SHAURI,WAWE NA HIARI KATIKA SHAURI LAO. NA MWENYE KAMUASI ALLAH NA MTUME WAKE, HAKIKA AMEPOTEA UPOTOFU ULIO WAZI (kabisa) [33:36]
Kuharamishwa uvaaji wa dhahabu kwa wanaume kumethibiti katika hadithi nyingi sahihi zilizopokelewa kutika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu –Rehema na Amani zimshukie.
1. Amepokea (riwaya) Imamu Bukhaariy, Muislam na Ahmad kwamba Mtume wa Allah “Amekataza (kuvaa) pete ya dhahabu”.
2. Imepokelewa kutoka kawa Ibn Abbaas-Allah awawiye radhi-kwamba Mtume wa Allah aliiona pete ya dhahabu kidoleni mwa mtu, akamvua na kuitupa (huku) akisema “ Mmoja wenu analikusudia kaa la moto na kulivaa mkononi?” Mtu yule akaambiwa baada ya kwenda zake mtume “ Itwae pete yako unufaike nayo. Akawajibu Wallah hapana, kamwe sitaichukua ikiwa aliyeitupa ni Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.” Muislam
3. Na katika jumla ya riwaya zilizopokelewa kwamba Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie amesema : “ Ye yote mwenye kumuamini Allah na siku ya mwisho basi asivae hariri wala dhahabu.” Al-musnad {Musnadul–Imam Ahmad}
HITIMISHO
“AMA YULE ALIYEASI NA AKAYAPENDA ZAIDI (maisha) YA DUNIA. BASI KWA HAKIKA JAHANAAM NDIYO ITAKAYOKUWA MAKAZI YAKE. NA AMA YULE ALIYEOGOPA KUSIMAMISHWA MBELE YA MOLA WAKE, AKAIKATAZA NAFSI YAKE NA MATAMANIO (maovu). BASI HUYO PEPO NDIO ITAKAYOKUWA MAKAZI YAKE”. {79:37-41}.
Ndugu yangu mpenzi, chagua na uamue sasa, uvae dhahabu kwa kupata starehe na burudani ya muda mfupi ya duniani huku ukisubiriwa na adhabu kali ya milele ya akhera au uishinde nafsi yako na kuacha kuvaa dhahabu ewe mtoto wa kiume ukapate starehe ya kweli, ya kudumu ya akhera.