Thursday 23 May 2013

SHEHA WA SHEHIA YA TOMONDO AMWAGIWA TINDI KALI !!!



VITENDO vya uhalifu vinavyoendelea kujitokeza hapa nchini kila kukicha huku mamlaka zinazohusika na suala la ulinzi na usalama zinaonekana kukaa kimya kwa kushindwa kudhibiti vitendo hivyo.

Hayo yamebainika baada ya sheha wa shehia ya Tomondo Mohammed Saidi (Kidevu) jana kumwagiwa tindi kali akiwa nyumbani kwake Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja.

Tukio la kumwagiwa kwa tindi kali sheha huyo lilitokea mnamo majira ya saa 2:30 usiku, wakati akiwa katika harakati za kuchota maji.

Akizungumza katika hospitali ya Mnazimmoja ambayo ndio anayopatiwa matibabu sheha huyo alisema kabla ya tukio hilo kutokea alitokea kijana mmoja ambae hakumfahamu na kusalimiana nae na baadae kumwagia.

Alisema mara baada ya kumwagia acid alimfukuza kijana huyo huku akimnadia mwizi lakini alishindwa kupata msaada wowote kutoka kwa wananchi.

Awali sheha huyo alikua akipokea vitisho kutoka kwa watu mbalimbali ambao hawafahamu, ambavyo vimeanza wakati wa chaguzi za wilaya za kuwapata wajumbe wa baraza la katiba.

Kwa upande wake wake Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mkadam Khamis amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kuwa Jeshi la Polisi litafanya uchunguzi wa kina na kuhakikisha kuwa wanawakamata wale wote waliohusika na tukio hilo.

kamanda huyo ameyasema hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu alipokuwa ofisini kwake Madema.

Pia ametowa wito kwa wananchi kutokujichukulia sheria mikononi mwao kwani mara nyengine hupelekea matatizo zaidi.

Nae Daktari anaempatia matibabu hospitalini hapo Dk Saidi Ali amesema kuwa sheha huyo amepata majeraha katika jicho la upande wa kulia ,kifuani na mgongoni na hali yake inaendelea vizuri huku akisisitiza kuwa ataendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo mpaka Serikali itakapoamuwa kama asifirishwe au la.

Mapema Makamo wa pili wa Raisi Balozi Seif Ali Iddi alifika hospitalini hapo na kulitaka jeshi la polisi kuchuku hatua za kisheria na kufanya uchunguzi wa kina ili kuhakikisha muhusika wa tukio hilo anakamatwa.

“Tukio hili si lakwanza wala si lapili kwani mwezi wa disemba mwaka jana katibu wa mufti shehe Suleiman suraga alikubwa na kadhia hiyo”alisema Balozi Seif.

Hata hivyo amesema serikali imesikitishwa sana na vikitendo hivyo vinavyoashiria uvunjifu wa amani huku akisema serikali itagharamia matibabu yake.
 — with King Sujae and 5 others.

No comments:

Post a Comment