Thursday 2 May 2013

DUA MUNATAKIWA KUHUDHURIA KWA WINGI WAISLAM WOTE !!!


Status Update
By Uamsho Zanzibar
Bismillahir Rahmanir Rahiim

TANGAZO LA DUA YA PAMOJA

Jumuiya ya UAMSHO na Mihadhara ya Kiislamu-Zanzibar inapenda kuwatangazia Waislamu wote wanawake na wanaume kua, kutasomwa DUA ya pamoja, siku ya Ijumaa tarehe 03 Mei, 2013 katika msikiti wa Kibweni Silver sand, mara baada ya sala ya Ijumaa insha Allah.

Lengo la DUA hii ni kumuomba Mwenyezi Mungu awape Shekhe zetu ithbati kwa dhulma wanazofanyiwa na kuwa na subira pamoja na familia zao katika wakati huu mgumu. Dua hii itasomwa vile vile katika mikoa yote ya Unguja na Pemba Inshaa Allah. Shime sote tuhudhurie.

TUNATAKA ZANZIBAR YETU HURU, YENYE MAMLAKA YAKE KAMILI, KITAIFA NA KIMATAIFA
WABILLAH TAUFIQ

UAMSHO MEDIA CENTER
17 Jamad Al-Akhar, 1434 – 01 Mei, 2013
Email: jumiki@hotmail.com
Facebook: Uamsho Zanzibar
Twitter: @Uamsho1

No comments:

Post a Comment