Monday 21 October 2013

INAUMA WEWE ,LAKINI BASI MUNGU ATALIPA ,SOMA HAPA ,

Waziri wa Kilimo wa Jamhuri ZA Muungano wa Tanzania yupo UK kwa mualiko wa Serikali ya UK, Lakini Kilimo sio suala la Muungano na katika msafara wake hakuna Mwakilishi wa Serikali ya Zanzibar ambayo imeunda hiyo Jamhuri.
Wenzetu wanasema hizi kero wanazisikiliza na kuzifanyia kazi, [Mashuduu]. Katika ziara hi kama msaaada wa wataalamu ama wa mali wote huishia Tanganyika chini ya koti la jina la Tanzania. Na hili ni moja tu ya mifano Elfu.
Mh Christopher Chiza atafanya mkutano hapo kwenye Ubalozi, hivyo kila mwenye nafasi ya kutaka kumsikiliza na pia kumuuliza Masuali anakaribishwa tarehe 23 mwezi huu. Saa kumi na Moja jioni majira ya UK
Ningependa mkajitokeza kwa wingi kama mnayo nafasi.

No comments:

Post a Comment