Wednesday 28 August 2013

VIJANA WASEMA POPOTE PALE AENDAPO TUKO NAYE !!!


Wananchi mbali mbali wa jimbo la Kiembe Samaki wameelezwa kusikitishwa kwao na kitendo kilichofanywa na halmashauri kuu ya CCM NEC ya kumvua uanachama mwakilishi wa jimbo hilo hivi karibuni.

Mazrui media ilifanya jitihada za kuwatafuta wananchi wa jimbo hilo ili kuweza kujua wameipokeaje taarifa hii.

Mmoja miongoni mwa waliowahi kushika nyadhifa ya katibu wa tawi ndani ya jimbo hilo Bwana Sleiman Haroub Sleiman amesema kitendo cha kufukuzwa Mansour kimefanywa na baadhi ya timu maalumu ndani ya chama hicho ambayo inapingana na Raisi mstaafu wa Zanzibar Amani Abeid karume.

Alisema kuwa ndani ya jimbo hilo kuna baadhi ya watu tena walio wengi sana hususani vijana walikuwa karibu sana na Mwakilishi huyo hivo kutokana na ukaribu wao hule lololote lile linaweza kutokea katika kipindi hichi ambacho nikigumu zaidi kwa wananchi wa kiembe samaki waliomchagua Mansur kuwa mwakilishi wao.

Alisema wananchi mbali mbali hivi sasa ni wazi kuwa wanalichukulia suala hili kuwa ni lakawaida ndani ya chama lakini mambo yanaweza kugeuka na kuathiri zaidi tofauti na tunavofikiria.

Kuhusu shutuma zinazosambazwa na baadhi ya watu kuwa Dodoma ni machinjio tu ya wazanzibar alieleza kuwa sio kweli inawezekana wanaofukuzwa wanakila sababu za kufanyiwa hivo.

Kwa upande alieleza kuwa yeye binafsi anaumwa sana na suala hili lakini yupo tayari kumuunga mkono kiongozi yoyote yule atakaeteuliwa na chama chake cha CCM ndani ya jimbo hilo.

Akifafanua kuhusu suala la kutokurudisha kadi za chama cha ccm sikumsaliti Mansour bali nikukiunga mkono chama chao kwani hata huyo Mansour aligombea kwa chama hicho hicho yeye yupo tayari kumuunga mkono kiongozi yoyote yule atakaependekezwa na chama.

Nae Katibu wa Vijana CCM katika jimbo hilo la kiembe samaki ambae hakutaka jina lake litajwe.
Alieleza kuwa hali ya kufukuzwa kwa Mansour imemuuma sana sana na aliposikia taarifa hii alikuwa chuoni Tunguu kutokana na hali yake kubadilika mara moja aliamua kutoka nje ya darasa na kushindwa kabisa kuendelea na masomo kwa siku hio.

Alisema kuwa kila mmoja anajuwa wazi kuwa chama kimekurupuka juu ya hili na kilitakiwa kitulize wananchi kwanza hata kama Mansour alikuwa na kosa ndani ya chama hicho,cha msingi zaidi wangetumia busara kwa kumuangali mtu wenyewe ana umuhimu gani ndani ya jimbo lake.



Hata hivyo licha ya mwakilishi huyo kuwa na msimamo wa kuwepo serikali tatu sikosa kisheria kwani hayo yalikuwa mawazo yake na hakuna asiejua kwamba Mansour hakuwa pekeake mwenye msimamo huo ndani ya CCM kwanini afukuzwe yeye tu.

‘’Mh,Mansour siku zote alikuwa karibu na vijana na alitusaidia kwa hali na mali unadhani leo ni mwakilishi gani au kiongozi gani atakaekuwa kama yeye ndani ya jimbo hili’’alieleza.

Nae Nassra Mwinyi Chumu ambae ni mkaazi wa jimbo hilo alieleza wazi kwamba yeye binafsi hakuridhishwa kabisa na kitendo hicho na yupo tayari kumfata Mansour popote pale atakapokwenda kwani tayari amekuwa msaada mkubwa kwa jimbo hilo.

Aidha kwa upande wao vijana wa Manour maskani iliopo Chukwani wamesema kwamba wao binafsi hawataki kusikia lolote isipokuwa wanasubiri kauli yake yeye mwenyewe atasemaje na watamfuata kwa halili yoyote hile.

‘’Unajua nini kaka jamaa alikuwa na moyo wa imani sana na mpenda watu wote hususan vijana hapa maskani petu palikuwa kama nyumbani kwake’’walieleza vijana hao ambao hawakutaka watajwe majina yao.

Kwa upande wake Bwana Mansour Yussuf Himed wakati akifanya mahojiano na kituo cha habari cha DW cha Ujerumani alisema kuwa kwa sasa bado ni mapema mno kutoa tamko lolote lakini yeye ameyapokea maamuzi yalioamuliwa na chama kama yalivotolewa na chama hicho.

Akieleza kuhusu suala lakuvuliwa uanachama na hali yakuwa Bababa yake ni mmoja miongoni mwa waasisi wa mapinduzi ameleza kwamba wenzake ndio wameamua kufanya hivo hivo hana budi kukubaliana nayo maamuzi hayo.

Alieleza kwamba nchi yoyote hile yenye kuheshimu sheria ni lazima katiba yake ikushanye mawazo ya wananchi wake katika utungwaji wa katiba na hatimae mawazo ya waliowengi kusikilizwa nanadhani hio ingekuwa busara zaidi.

Licha ya hayo Mansour alifafanua kwamba muda ukifika atasema hadharani kwani ana mingi yakusema.

No comments:

Post a Comment