Thursday 13 February 2014

VIONGOZI WAJIZANA DR BILAL V/S WARIOBA


Leo kuna kikao kinaendelea katika Hoteli ya White Sands , ambacho KIMEANDALIWA na TCD , ambacho kimepewa jina la "Mkutano wa Tafakuri na Maridhiano kuelekea Katiba Mpya" ambacho kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Bunge na Vyama vya Siasa , Viongozi wa Dini, wabunge wapya wa Bunge la Katiba na Tume ya Mabadiliko ya Katiba .

Baadhi ya Viongozi wa Kitaifa waliohudhuria ni pamoja na Dr.Gharib Bilal, Mizengo Pinda, Anne Makinda, Pandu Kificho,Joseph Warioba,Pius Msekwa, Philip Mangula,Freeman Mbowe, Dr.Wilbroad Slaa, Prof.Lipumba, James Mbatia,Stephen Wassira, Asha Rose Migiro,Mathias Chikawe, Askofu Mokiwa, Amir Kundecha,Butiku na wengineo wengi wa aina hiyo.

Joseph Warioba

katika kikao hicho aliyetegemewa kufanya hotuba yaUfunguzi ni Rais Kikwete, ila badala yake alimtuma Bilal kumwakilisha, ndipo katika hotuba yake ya ufunguzi alipoishambulia tume ya Warioba na kuweka msimamo kama ifuatavyo;

1. Kuwa tume haikutumwa kwenda kuandaa rasimu itakayopendekeza uwepo wa serikali tatu , hivyo hayo ni mambo ambayo tume ilijitungia yenyewe , na hivyo Bunge la katiba litaenda kufanya uamuzi kwa misingi ya KURA .....na kila mmoja ajiandae kupokea maamuzi ya kura , hata kama yataenda kinyume na mawazo ya tume ya Warioba .

2. Wao hawakutumwa kwenda kupunguza mambo ya Muungano bali ni kwenda kuyaongeza kama vile suala la Afya, Elimu yalipaswa kuongezwa kwenye rasimu hiyo , ila tume imeenda kuyapunguza , hivyo wanatishia uhai wa Muungano na hivyo ni mawazo ambayo hayapaswi kuungwa mkono na mtu yeyote mwenye akili timamu.
3. Kongamano , limeandaliwa kwa lengo la kupigia debe mawazo ya wakina Warioba ambao ni kikundi kidogo katika jamii na ambao hawawakilishi mawazo ya wengi.

Baada ya maneno hayo na mengine mengi alifungua mkutano , na akitaka kuondoka ila aliombwa anakiri ili aupate majibu kutoka tume na ili asiwe wa kwenda kuambiwa nini kimesemwa , ndipo Warioba alipomuoa kumjibu kwa hoja na vielelezo vya kutosha kuhusu walivyoweza kufikia kwenye HITIMISHO la kuwepo kwa Serikali tatu
MAJIBU YA WARIOBA YALIKUWA KAMA IFUATAVYO !
1. Wao walichofanya ni kukusanya maoni ya wananchi na kuyachambua , na hivyo kutengeneza rasimu kutokana na maoni yao na sio kuwa walijifungia na kuanza kuandika maoni yao binafsi 
2.Wananchi ambao walipendekeza muundo wa Muungano ni kuwa asilimia 4% walisema Muungano usiwepo, 13% walisema uwe wa serikali moja , 22% walisema Muungano wa serikali tatu na 61% walisema kuwa Muungano uwe wa serikali tatu, hivyo kiongozi kusema kuwa tume imejitungia ni kutokujipa muda wa kutazama video na nyaraka mbalimbali walizopewa kama vielelezo vya maoni ya wananchi.

3. Kuwa serikali ya Muungano , imejivika koti la Muungano wakati ikiwa inajishughulisha zaidi na mambo ya Tanganyika , ndio maana Waziri Mkuu hajawahi kwenda Zanzibar kufanya shughuli za kimaendeleo wala kukagua miradi ya maendeleo huo , kwani anajiona yeye ni wa Tanganyika, pia alisema kuwa ukitazama Bunge la Muungano , maswali asilimia 90 yanayoulizwa ni kuhusu mambo ya Tanganyika , kuliko ya Muungano, bajeti ya Muungano asilimia 80 inashughulika na mamb ya Tanganyika kuliko mambo ya Muungano, ndio maana hakuna pesa inatengwa kwa ajili ya maendeleo ya zanzibar , hakuna mtu anajiuliza Zanzibar utapata wapi fedha za kujiendesha nk.

4. Zanzibar ni nchi na katiba yao imepuuza kabisa uwepo wa serikali ya Muungano , ndio maana katiba yao inasema kuwa wao ni nchi na wana Wimbo wa taifa, bendera nk , hivyo kuendelea kujidanganya kuwa Muungano wa serikali mbili upo ni kujivika Tabia za mbuni.......

5. Tume ili pitia ripoti ambazo waliochukua kwenye ofisi ya makamu wa Rais kama vile ripoti ya kamati ya Amina, Shelukindo, Kisanga nk kuhusu Muungano na kote huko kuna malalamiko juu ya Tanganyika kujivika koti la Muungano , nashangaa hata waziri mkuu hapa aliposema Zanzibar sio nchi mnakumbuka yaliyokumkuta huko Bungeni.....

Pius Msekwa, amemuunga mkono Warioba na Kumtaka Wassira ajenge hoja ni kwanini serikali mbili ni muhimu , na sio kuishia kuwa na Mazoea kuwa tumezoea hivi , fear of the unknown....na pia hata hati za Muungano ziliweka wazi kuwa serikali mbili ilikuwa ni kwa interim period only.....sasa je ? Tuendelee kuwa kweye hai hyo baada ya miaka50

Hayo ni ni baadhi ya mambo yalivyo kuwa kwenye kikao na bado kikao kinaendelea 

No comments:

Post a Comment