Monday 8 June 2015

AKAAA AKUTANA NA MEYA RAIS WA NCHI ?AMA KWELI WAMESHAUZWA WAZANZIBAR

Hapa ndipo Zanzibar tulipofikishwa katika mfumo wa Muungano uliopo. Rais wa Zanzibar anakwenda katika ziara tuliyoambiwa ni ziara rasmi nchini Ujerumani lakini anaishia kukutana na Meya wa Wurzburg.
Zanzibar iliyokubali kuchanganya (na siyo kusalimisha) mamlaka yake kuhusu mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa na Tanganyika ili yasimamiwe kwa pamoja na inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi na manufaa ya nchi zote mbili (Zanzibar na Tanganyika) leo haiwezi kutumia fursa zilizopo kuinua uchumi wake na kubadilisha maisha ya watu wake.
Tanganyika imevaa koti la Muungano na inazitumia kikamilifu fursa zote za mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa na Zanzibar inaishia kutembelea Meya. Ubalozi wa inayoitwa Jamhuri ya Muungano ambao unapaswa kuzihudumia Zanzibar na Tanganyika kwa usawa umeshindwa kusimamia maslahi ya Zanzibar na badala yake unaendeleza mahusiano ya kimataifa kwa maslahi ya Tanganyika tu. Huu si Muungano; ni Ukoloni.
Madalali wa CCM Zanzibar wanasema mfumo huu ndiyo unaoifaa Zanzibar na wakaona fakhari kutuuza Dodoma. Wazanzibari tutafanya maamuzi ya kuwahukumu Madalali hawa Oktoba 25, 2015. Lugha ni moja tu: DELETE, FUTA KABISA

No comments:

Post a Comment